Proverbs 29:2-7


2 aWenye haki wanapostawi, watu hufurahi;
waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.


3 bMtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake,
bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.


4 cKwa haki mfalme huipa nchi uthabiti,
bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.


5 dYeyote amsifuye jirani yake isivyostahili,
anautandaza wavu kuitega miguu yake.


6 eMtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe
bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.


7 fMwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini,
bali mwovu hajishughulishi na hilo.

Copyright information for SwhKC